BREKING NYUUUZZZZZ: kocha athumani kilambo afariki dunia usiku huu

Marehemu Athumani Kilambo (kanzu ya kijani) enzi za uhai wake akiwa na wakongwe wenzie wa Pan African Saad Mateo (kushoto) na Kitwana Manara (wa pili kulia). Kocha Athumani Kilambo akiwa na kikosi cha Pan Africa kilichonyakua ubingwa 1982
Marehemu Athumani Kilambo (wa pili nyuma kushoto) akiwa na kikosi cha Yanga kilichotembelea Brazil mwaka 1974. Hapa ni uwanja wa Maracana
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema mchezaji huyo wa zamani wa Yanga na kocha wa Pan Africa amefariki dunia usiku huu baada ya kusumbuliwa na saratani ya koo kwa takriban miaka miwili. Hivi majuzi alitolewa hospitali ya Ocean Road jijini Dar es salaam alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya majuma mawili. Msiba uko nyumbani kwake Mwananyamala B Kwa Mama Zakaria
Source: ISSA MICHUZI
Previous Post Next Post