Waandishi wa habari nchini wameaaswa kuachana na matumizi pekee ya internet kuandika habari badala yake kutafuta habari kwa uasilia badala kuchukua nhabari za mitandao
misa tan kwa ufadhili wa mfuko wa vyombo vya habari,mawasiliano na maendeleo Finland yanayoendelea katika ukumbi wa chuo kikuu cha stella
maris mkoani Mtwara.
LIcha kwa kuwepo kwa njia rais ya upatikanaji wa habari kupitia mitandao ya internet hapa nchini waandishi wametakiwa kufuatilia habari halisia kuepukana na kuwepo na mitandao ya uongo inayopotosha jamii.
Kwa upande wake mratibu wa mafunzo hayo Andrew Marawiti kutoka Misa Tanzania akieleza malengo ya mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa matumizi ya internet katika upatikanaji wa habari mbalimbali na ualisia wake ili kuepuka na mitandao inayolenga kupotosha jamii. Jumla ya waandishi wa habari 20 kutoka mikoa ya lindi na mtwara
wanapata mafunzo ya matumizi ya internet yanayotolewa na Taasisi ya maendeleo ya Habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania(MISA TANZANIA) chini ya Ufadhili wa Mfuko wa vyombo vya Habari,Mawasiliano na Maendeleo Nchini Finland (VIKES FOUNNDATION)
HABARI NA AHMEID ABDULAZIZ