Washabiki wa mpira Misri wakasirika

Mapigano yamezuka katika mji wa Port Said nchini Misri na kijana mmoja amekufa, baada ya timu ya mji huo kupigwa marufuku kwa miaka miwili kufuatia ghasia za mwezi Februari, zilizouwa watu zaidi ya 70.Washabiki wa Port Saidi wakipambana na polisi mwezi Februari

Mamia ya washabiki wa klabu hiyo ya al-Masry walipambana na askari wa usalama walipozingira jengo la serikali, kulalamika juu ya timu yao kupigwa marufuku.

Inaarifiwa kuwa polisi walitumia moshi wa kutoza machozi na kufyatua risasi hewani.

Adhabu hiyo ya klabu ya al-Masry kukatazwa kucheza kwa miaka miwili, imetokana na ghasia zilizozuka katika uwanja wa timu hiyo ilipopambana na al-Ahly ya mjini Cairo.

Wamisri wengi wanawalaumu askari wa uslama kwa kutozimua ghasia za mwezi Februari.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post