Msanii wa Bongo flava na mkali wa ngoma ya Bongo flava, Dully Sykes a.k.a Mr Misifa alikamatwa na polisi baada ya kuvamia msafara wa Rais bila yeye kujua, alikua kasi sana
hakujua kama kulikua na msafara huo, Alipopita akasimamishwa na polisi wakakoki bunduki tayari kwa ajili ya kushambulia gari hilo ili kuepusha chochote ambacho kingeweza kutokea kwa rais, Dully akaenda mbele
akapark petrol station nakushuka akamkamata nakumhoji ndipo akasema hakujua na alikua anawahi sana baada ya mtu aliekua anamlipa pesa zake baada ya kufanya tangazo la kinywaji.
“ Ilibidi niwahi sana baada ya jamaa kuniambia anataka aondoke na anazo pesa zangu” Alisema Dully. Alipokaguliwa akakutwa na
makosa mawili la kwanza kuendesha bila leseni ambayo alikua ameiacha nyumbani Dully anasema pamoja na Insurance ya gari ilukua
imeisha muda wake.