Mwimbaji DIAMOND PLATNUMS, amefikishwa leo asubuhi kwenye MAHAKAMA ya MWANZO BOMANI mjini Iringa kwa ajili ya kesi ya kumpiga na kumuharibia vifaa mwandishi wa habari Francis Godwin. Mwandishi huyo wa habari amesema asingemfikisha DIAMOND mahakamani kama angekubali kumuomba msamaha, lakini kwa sababu hakukubali kufanya hivyo ndio maana akaamua kumfungulia kesi. wiki iliyopita, Mwandishi huyo alikataa kupokea shilingi milioni 1.7 alizotumiwa na DIAMOND kama fidia ya vifaa vyake na badala yake akataka aombwe msamaha na DIAMOND mwenyewe, na sio kumtuma mtu.
Karandinga ambalo Diamond ametumia kufika mahakamani ni gx 100.
Mdhamini wa msanii DIamond Edo Bashir Kushoto akizungumza na Francis Godwin ambaye ndie mlalamikaji katika kesi hiyo
Tags
HABARI ZA WASANII