NIJUZE NIJUZE Author
Title: Boas asema matokeo na United si muhimu
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Kocha wa Chelsea Andre Villas-Boas amesema matokeo ya mechi kati ya Chelsea na Manchester United siku ya Jumaapili "hayatamaanisha choc...

imageKocha wa Chelsea Andre Villas-Boas amesema matokeo ya mechi kati ya Chelsea na Manchester United siku ya Jumaapili "hayatamaanisha chochote kwani ni mapema sana kuleta athari yoyote kwa mchuano wa ligi."

"Umuhimu wetu katika mchezo huo ni mdogo mno. Ni juu ya wachezaji kutumia umahiri wao na kufurahia mchezo wao. Kocha yeyote atakayehukumiwa baada ya mechi tano tu inamaanisha kasoro haziko kwa kocha bali kwa watu wanaosimamia vilabu."

Kushindwa kwa Chelsea kutaiweka klabu hiyo pointi tano nyuma ya Manchester United, lakini wakishinda wataipiku United kwa pointi moja zaidi.

Mechi hii inawakutanisha mojawapo wa makocha wa muda mrefu, Ferguson dhidi ya mojawapo wa makocha vijana kabisa ,Villas-Boas.

Villa Boas alikua na umri wa miaka 9 wakati Sir Alex Ferguson alipochukua hatamu za kuinoa Manchester United.

Kwa mara nyingine Chelsea haitamchezesha Didier Drogba, ambae alipoteleza fahamu wakati Chelsea ilipoishinda Norwich wiki tatu zilizopita. Kwa hiyo kocha Villas-Boas itampasa aamuwe kama kuanza na Fernando Torres ama Nicolas Anelka.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top