El Classico ndani ya Tuzo za Mchezaji Bora Ulaya

image

Upinzani baina ya Real Madrid na Barcelona maarufu kama “El Classico” umeamia kwenye tuzo za mchezaji bora barani ulaya baada ya Cristiano Ronaldo, Lionel Messi na Xavi Hernandez kuchaguliwa kugombea tuzo hiyo.

Tuzo hizo zimepangwa kufanyika mwezi ujao baada ya wachezaji hao watatu kuchaguliwa na waandishi wa michezo 53 kutoka katika kila mwananchama wa UEFA katika listi ambayo pia imewahusisha Wayne Rooney na Andres Iniesta.

Kura za kuchagua mchezaji bora atakayeshinda tuzo hiyo zitapigwa August 25.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post