HAMISA MOBETTO ATOBOA SIRI USIO IJUA KUHUSU YEYE NA ZARI THE BOSSLADY

Hamisa Mobetto amefunguka juu ya mahusiano yake na first lady wa Madale, Zari The Bosslady baada ya tetesi za kutoka na Diamond.
Hamisa Mobetto
Mrembo huyo amemuambia mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Omary Tambwe aka Lil Ommy kuwa hajawahi kuwa na urafiki na Zari na wala hawana uadui wowote.
“Unajua huwezi kusema kuwa mimi na Zari tuko sawa au hatupo sawa kwa sababu hatujawahi kuwa marafiki, na mimi nimemjua kwa sababu ‘Kazaa’ na bosi wangu [Diamond Platnumz],” amesema Hamisa.
Malkia huyo wa video ya Salome ameongeza kuwa amewahi kuonana na Zari mara moja pekee ambapo ilikuwa ni kwenye 40 ya Tiffah mwaka jana.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post