RAIS MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKUU HUYU WA WILAYA

Juni 26 mwaka huu Rais John Pombe Magufuli alitangaza kuteua Wakuu wa Wilaya zote nchini, na Wakuu wa Mkoa watatu. Kati ya Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa, 39 wamebakishwa katika nafasi zao huku 100 wakiwa ni wapya.
Rais Magufuli
Katika hali ya kushangaza siku moja baada ya orodha hiyo kutangazwa, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa wilaya ya Ikungi iliyopo mkoani Singida. Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Bwana Fikiri Avias Said ndani ya masaa 24 tangu uteuzi wake.

Sababu kuu ya Rais kutengua Uteuzi huu ameisema leo hii wakati wa hafla ya kuwaapisha Wakuu wote walioteuliwa, ni kwamba jina lilikosewa, na kusema kwamba Mkuu wa Wilaya halali wa Ikungi ni Bwana Miraji Mtaturu ambaye ni Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mwanza,

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post