IJUMAA JULY 1, 2016 ONGEZEKO LA ASILIMIA 18 (VAT) YA MAKATO YA MIAMALA YA KIBENKI KUANZA KUTUMIKA

Ijumaa hii itakuwa tofauti kwa wateja wengi wa benki nchini. Ni kwasababu benki karibu zote kuanzia July 1, zitaanza kutumia sheria mpya ya fedha ya mwaka huu iliyopitishwa na bunge la 2016/17.
CRDB
Kupitia tangazo lake kwa wateja, benki ya CRDB imedai kuwa ongezeko la asilimia 18 zitatozwa katika gharama za huduma ya benki kuanzia Ijumaa hii, July 1.

“Ongezeko hili (VAT) litakatwa kutoka katika akaunti na kama muamala hautapita kwenye akaunti, mteja atalipia kwa fedha taslimu, Kulingana na sheria hii, hakutakuwa na makato ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT) katika riba,” imesema taarifa hiyo.

Benki ya NMB nayo imetoa taarifa hiyo kwa wateja wake.
NMB

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post