"SURPRISES" ZILITAWALA TUZO ZA WATU 2015, ANGALIA PICHA HAPA

Tuzo za watu 2015 zimetolewa Ijumaa hii kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa ‘surprises’ za kutosha. Mshindi mkubwa kwenye usiku huo na ambaye amekuwa surprise kwa wengi ni mtangazaji wa TBC FM, D’jaro Arungu aliyeibuka na tuzo mbili.
Millard Ayo na Salim KikekeMillard Ayo na Salim Kikeke

D’Jaro alikuwa akishindana na Millard Ayo kwenye vipengele hivyo viwili ambaye hata hivyo alishinda pia kipengele cha blog inayopendwa.

D’Jaro ArunguD’Jaro Arungu akiongea baada ya kutangazwa mshindi

“Mtu yeyote aliyekuwa anashindani halafu anaamini anaweza kupata nafasi lazima imshtue,” Millard ameiambia Bongo5.

Millard AyoMillard Ayo akipokea tuzo ya blog inayopendwa

“Lakini inakushtua kwa njia nzuri kwamba kuna kitu kimemiss au labda unatakiwa ufanyie kazi zaidi. Lakini pia kura zinamata, inachangia sehemu zote, inawezakana ubora wa kipindi na kura pia. Lakini all in all mimi nampongeza sana D’Jaro Arungu, ameshinda kura zote mbili, ni changamoto pia, inatupa nafasi sisi wenyewe kushindana lakini inasaidia pia kufanya kazi kwenye biashara yetu vizuri.”

Wema Sepetu aliyekuwa ametajwa kuwaniwa vipengele vitatu ameibuka na tuzo moja.

Wema Sepetu Wema Sepetu akipokea tuzo yake ya muigizaji wa filamu anayependwa

“I’m Grateful… I’m humbled…. I’m out of words… Ila nawapenda for making this happen…. Shout out to all my fans out there… Na haters pia…. I say it’s a new beginning.”

“Therez more to this…. I take it as a challenge and a wake up call to give you guys more of what you want me to give,” ameandika Wema kwenye Instagram baada ya ushindi huo,” aliongeza Wema.

Ray Ray akishukuru baada ya kutangazwa mshindi wa kipengele cha muongozaji wa filamu anayependwa
Dada wa Alikiba
Dada wa Alikiba akipokea tuzo kwa niaba ya kaka yake
Lady Jaydee
Lady Jaydee akishukuru baada ya kushinda tuzo ya mwanamuziki wa kike anayependwa
Ommy DimpozMiss Tanzania 2014/15, Lilian Kamanzima akimkabidhi tuzo Ommy Dimpoz
tuzo za watu 2015
Shangwe kwa washindi
Jacqueline Mengi na Nasreen KarimJacqueline Mengi na Nasreen Karim ni miongoni mwa waliohudhuria
Luca na Nancy
Luca na Nancy wakizungumzia tuzo za watu 2015

Hii ni orodha kamili ya washindi

Mtangazaji wa redio anayependwa

D’Jaro Arungu – TBC FM

Kipindi cha redio kinachopendwa

Papaso – TBC FM

Mtangazaji wa runinga anayependwa

Salim Kikeke – BBC Swahili

Kipindi cha runinga kinachopendwa

Mkasi – EATV

Blog/Website inayopendwa
Millardayo.com

Muongozaji wa video anayependwa
Hanscana

Muongozaji wa filamu anayependwa
Vincent ‘Ray’ Kigosi

Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa
Wema Sepetu

Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa
Hemedy PHD

Mwanamuziki wa kike anayependwa
Lady Jaydee

Mwanamuziki wa kiume anayependwa
Alikiba

Filamu inayopendwa
Kigodoro

Video ya muziki inayopendwa

Nani kama Mama – Christian Bella f/ Ommy Dimpoz

>>BONGO5
Previous Post Next Post