Mshambuliaji Cristiano Ronaldo ameondolewa adhabu ya kutocheza mchezo wa mwishoni mwa juma hili baada ya rufaa ya uongozi wa Real Madrid kufanikiwa.
Kanuni za ligi ya nchini Hispania zilikua zinambana Ronaldo kucheza katika mchezo wa kesho dhidi ya Eibar, kutokana na kufikisha idadi ya kadi tano za njano, mara baada ya mchezo wa siku mbili zilizopita ambapo Real Madrid walichomoza na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya Rayo Vallecano.
Uongozi wa Real Madrid uliwasilisha rufaa ya kupinga maamuzi yaliyochukuliwa na muamuzi aliyechezesha mchezo dhidi ya Rayo Vallecano, sambamba na ushahidi wa tukio la kuanguka katika eneo la kisanduku cha penati ambapo alidhaniwa alifanya makusudi.
Kamati ya mashindano iliyo chini ya shirikisho la soka nchini Hispania imejiridhisha kutokana na ushahidi, na imebainika Ronaldo hakujiangusha kwa makusudi bali alichezewa ndivyo sivyo na beki wa Rayo Vallecano, Antonio Amaya katika dakika ya 51.
Kwa mantiki hiyo sasa Ronaldo atakuwa sehemu ya kikosi cha Real Madrid kitakachoshuka kwenye uwanja wa nyumbani hiyo kesho kupambana dhidi ya Eibar.
Uongozi wa Real Madrid uliwasilisha rufaa ya kupinga maamuzi yaliyochukuliwa na muamuzi aliyechezesha mchezo dhidi ya Rayo Vallecano, sambamba na ushahidi wa tukio la kuanguka katika eneo la kisanduku cha penati ambapo alidhaniwa alifanya makusudi.
Kamati ya mashindano iliyo chini ya shirikisho la soka nchini Hispania imejiridhisha kutokana na ushahidi, na imebainika Ronaldo hakujiangusha kwa makusudi bali alichezewa ndivyo sivyo na beki wa Rayo Vallecano, Antonio Amaya katika dakika ya 51.
Kwa mantiki hiyo sasa Ronaldo atakuwa sehemu ya kikosi cha Real Madrid kitakachoshuka kwenye uwanja wa nyumbani hiyo kesho kupambana dhidi ya Eibar.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.