Nani amevieleza vyombo vya habari kwamba kusajiliwa kwa mkopo kwenye klabu ya Sporting Lisbon ni sehemu ya kutaka kumthibitishia meneja wa Man Utd Louis Van Gaal kama ana uwezo wa kuendelea kuwepo kwenye kikosi chake na si kufunguliwa milango ya kuondoka Old Trafford.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27, amesema hakuumizwa na kitendo cha kupelekwa kwa mkopo kwenye klabu ya Sporting Lisbon na ndio maana anaitumikia klabu hiyo kwa moyo wake wote.
Amesema anajua mashabiki wengi wanaamini huenda ikawa mwisho wake kucheza soka akiwa na Man Utd, lakini kwake anaamini bado ni mchezaji halali wa klabu hiyo na mwishoni mwa msimu huu atarejea kwa ajili ya kuendeleza mipango ya kuisaidia klabu hiyo iliyomsajili mwaka 2007.
Luis Nani alilazimika kuondolewa kwenye kikosi cha Man Utd mwanzoni mwa mwezi huu na kupelekwa kwa mkopo kwenye klabu ya Sporting Lisbon ya nchini kwao Ureno baada ya kushindwa kumridhisha kiuwezo wa soka meneja wa Man Utd Louis Van Gaal.
********************************************
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.