RC AWATAKA WADAU WA ELIMU KUTIMIZA WAJIBU

Ludovick Mwananzila Mkuu wa Mkoa wa Lindi 
(picha na Maktaba)

Na. Mwanja Ibadi..Lindi
Mkuu wa mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila amewataka Wadau elimu  mkoani humo  kutambua umuhimu wa elimu kwa kuwapeleka watoto wao shuleni ili waweze kupata haki yao ya msingi ya kupata elimu ambapo  itawasaidia kuweza kuwa na maisha bora ya baadaye.
 
Agizo hilo amelitoa kwenye  kikao cha wadau elimu mkoa wa Lindi kilichofanyika  kwenye ukumbi wa Kagwa jana.
 
Mwananzila alisema Moja ya haki za watoto wanazotakiwa kupewa ambazo zimeainishwa katika sera na mipango mbalimbali ya serikali ni kupata haki ya elimu kwa kuwa elimu ni ufunguo wa maisha na rasilimali pekee ambayo itaweza kumfanya aweze kuwa na uhakika wa kuweza kujitegemea katika maisha yake ya baadaye.
 
Alisema iwapo mzazi ama mlezi atashindwa kumpeleka mtoto wake shuleni kwa sababu ambazo si za kimsingi hatakuwa anamnyima haki ya kupata elimu na kwamba uwezekano wa mtoto kuwa na maisha yasiyo na uhakika ni mkubwa na kwamba taifa litakuwa na kizazi kisichokuwa na uwelewa.
 
“Kwa maisha ya sasa niwakumbushe wazazi na walezi kuwa hakuna rasilimali kubwa kwa mtoto anayotakiwa kupewa isipokuwa elimu…elimu ndio rasilimali ambayo mtoto anatakiwa kurithishwa na mzazi hivyo wazazi tuzingatie umuhimu wa kuwapatia elimu watoto wetu ili waweze kujikomboa kimaisha ya baadaye,”alisema Mwananzila
 
Mwanazila alisema  kuwa changamoto kubwa iliyopo katika jamii ni kwamba uwelewa mdogo kuhusu umuhimu wa elimu  hali inayochangia baadhi ya wazazi na walezi kushindwa kuwapelaka watoto wao shuleni lakini kupitia elimu wanayoitoa imesaidia kuifanya jamii kuanza kuwa na mwamko wa kuzingitia suala la elimu.
 
Alisema kwa kulitambua ili mkoa umepanga mikakati mbalimbali ikiwemo ya kufanya vikao kwa kujadili changamoto hizo  kwa kuzitafutia majibu
 
Awali katibu tawala mkoa wa Lindi Abdala chikota  aliwataka wadau hao kutambua kuwa wajibu kusimamia na kutekeleza  majukumu ya maendeleo ya mkoa yatafanywa na wadau wanaopenda maendeleo katika mkoa huyo.
 

Chikota Alisema kushuka au kupanda kwa kiwango cha taalumu kunategemea kuwajibika kwa wadau kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto na kutengeneza miundombinu  rafiki kwa watendaji wakiwemo walimu.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post