Unknown Unknown Author
Title: MAMA KIKWETE AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA LINDI KUTUNZA AMANI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mama Salma Kikwete Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi Wakazi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kutodanganyika na kundi la watu wachache wanaotaka k...

clip_image001Mama Salma Kikwete

Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi

Wakazi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kutodanganyika na kundi la watu wachache wanaotaka kuvuruga amani iliyopo bali waitunze na kuhakikisha kuwa haipotei kwani amani ikitoweka hao wanaowadanyanga watakimbia na kuwaacha wakiteseka .

Wito huo umetolewa jana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa wakati wa uzinduzi wa sherehe za kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinnduzi (CCM) mkoani Lindi zilizofanyika katika kata ya Kiwalala wilaya ya Lindi vijijini ambapo chama hicho kinatimiza miaka 37.

Mama Kikwete alisema CCM imefanya mambo mengi katika harakati za ukombozi Barani Afrika kwani Tanzania ilikuwa kimbilio la wanyonge kwa kuwa wapigania uhuru wengi kutoka nchi za Kusini mwa Afrika ambazo hazikuwa zimepata uhuru walipokelewa , walihifadhiwa , walisaidiwa na kuwakarimu kwa dhati jambo ambalo si dogo na hii yote ilitokana na amani iliyopo.

“Chama chetu kimefanya  mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuleta Demokrasia ya vyama vingi toka mwaka 1992 na leo hii tunatimiza miaka 22 ndani ya mfumo wa vyama vingi huku tukiwa na amani, umoja na ushikamano miongoni mwa watanzania, tumeleta usawa kwa wananchi wote bila kujali jinsia, rangi kabila wala dini.

Chama cha Mapinduzi kupitia Serikali zake zinawajali wananchi kwa kuwasogezea huduma mbalimbali za kijamii hadi vijijini  na kupanua fursa za kiuchumi na kimaendeleo kwa wananchi”, alisema Mke wa Rais.

Aidha Mjumbe huyo wa NEC  pia aliwataka wananchi hao kujishughulisha na  kazi mbalimbali  za maendeleo ikiwa ni pamoja na kulima  japo mazao ya chakula kama muhogo kwani Serikali tayari imeshafanyia mambo mengi ya maana ambayo yanawasaidia  katika shughuli zao za maendeleo.

Mama Kikwete alisema, “Serikali imejenga Shule, Hospitali, barabara na kuimarisha miundombinu ya barabara  na leo hii kama mtalima kwa bidii mtaweza kusafirisha na  kuuza mazao yenu mbali na hapa kwakuwa barabara ni nzuri na usafiri ni wa uhakika”.

Kwa upande wake Mlezi wa Chama hicho katika mkoa wa Lindi Dk. Maua Daftari aliwataka wanachama wa chama hicho kuwa na umoja na mshikamano kwa kufanya hivyo wataweza kushinda na kutekeleza ilani ya chama chao.

Katika uzinduzi wa sherehe hizo ambazo  kilele chake kitafanyika  leo katika wilaya ya Ruangwa jumla ya wanachama 17 walijiunga na chama hicho ambapo wanachama wapya ni 12,  kutoka chama cha upinzani cha Civic United Front(CUF) wanne na  Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mmoja.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top