Kwa zaidi ya wiki moja iliyopita habari zilisambaa kwamba binti Mtanzania aliekamatwa na dawa za kulevya nchini Misri angenyongwa siku za karibuni kutokana na hizo dawa alizokamatwa nazo.
Baadae Balozi wa Tanzania Egypt ambae alikanusha taarifa za kunyongwa na akakubali kwamba kweli kuna Watanzania wawili wamekamatwa ambao ni huyo msichana na ndugu yake wa kiume ambao ni wakazi wa Magomeni Dar es salaam na kwamba wanashikiliwa na polisi huku wakisubiri kesi yao.
Leo hii, pata nafasi kuona video ya mahojiano ya TV na msichana huyu ambae anadai alikwenda Misri kumtafuta binamu yake, begi alilokamatwa nalo ni lake ila alikua hajui kama lina dawa za kulevya.
Inaanza na kiarabu baadae anahojiwa kwa kiingereza adai yeye ni Muoman na mama yake ni Mtanzania SIKILIZA MAHOJIANO
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.