ONYESHO LA MWISHO KATIKA TAMTHILIA YA SIRI YA MTUNGI MSIMU WA KWANZA

Katika onyesho la mwisho la msimu wa kwanza, kisasi ni kitamu kwa Farida pale anapotonywa habari nyeti toka kwa fundi cherehani, Furaha.
Wakati Mwanaidi anamkabili mkwewe kuhusiana na picha chafu alizompiga Lulu, Cheche anajitetea kwa nguvu kuwa hana kosa.
Wakati fulani Duma anakumbana na Nusura mja mzito akielekea kliniki. Hawezi kuvumilia kumwona akiwa na Mzee Kizito.
Kipindi hiki, Nusura anapata habari ambazo zitayabadilisha maisha yake milele. Na kule kwenye studio ya picha, umbo kutoka nyakati zilizopita, linaibuka kutokea kusikojulikana na kuutikisa ulimwengu wa Cheche.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post