Kinyang'anyiro ni kikali kati ya Muungano wa Cord na Jubilee wa Raila Odinga na Uhuru Kenyatta.
Kwenye ukurasa huu tutakupasha matukio kila yanapojiri hadi upigaji kura utakapokamilika mwendo wa saa kumi na moja jioni.
Unaweza kututumia maoni yako kuhusu uchaguzi kwenye ukurasa wetu wa facebook
18:22: Mwandishi wa BBC Jamuhuri Mwavyombo
amesema kuwa kulika na matatu tofauti, mjini Mombasa ambako kundi la MRC
linaendesha harakati zake. Mashambulio mawili, yalifanyika mtaa wa
Changamwe, ambako polisi walishambuliwa na tukio la tatu katika kituo
cha polisi eneo la Chumani Kilifi.
16:27 :Sehemu nyingi za starehe
na ulevi mjini Nyeri Mkoa wa Kati zimefungwa na zitafunguliwa Jumanne
ili kuwaruhusu wapiga kura kupiga kura. Eneo la Mkoa wa Kati lina tatizo
la uraibu wa pombe
16:24: Ng'endo Angela
ambaye yuko Mkoa wa Kati anasema kuwa kuwa sababu ya hitilafu za
kimitambo, tume imelazimika kutumia mfumo wa kawaida kwa kutumia daftari
za wapiga kura. Ni Nyeri peke yake ambako shughuli hiyo ilifanikiwa kwa
njia ya Elktroniki
15:54 Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza
anasema kuwa foleni mjini Nakuru zimeanza kupungua na huenda wapiga
kura wakamaliza shughuli hiyo itimiapo saa kumi na moja jioni muda wa
mwisho wa kupiga kura
15:16 Mmoja wa wagombea wakuu wa urais Uhuru Kenyatta
ameelezea maskitiko yake kuhusu yaliyojiri Mombasa ambako washukiwa wa
kundi la MRC waliwaua polisi na raia katika mashambulizi usiku wa
kuamkia leo. Lengo lao lilikuwa kuvuruga shughuli ya uchaguzi
14:57 Mwandishi wa BBC mjini
Kisumu Ann Mawathe anasema milolongo ya watu imepungua sana katika
sehemu nyingi za mji huo ikizingatiwa kuwa asubuhi watu walikuwa wamejaa
pomoni
14:51 Kuna taarifa kuwa magari ya Abiria yameanza kuongeza nauli ya magari kwa sababu ya upungufu wa magari hayo wakati wakenya wakiwa wamejitokeza kupiga kura
13:33 Tume ya uchaguzi imeagiza uachaguzi kurejelewa katika wodi tano kati ya zote 1'450 ambako mitambo ya tume hiyo ilikumbwa na hitilafu pamoja na makosa kwenye karatasi za kupigia kura
13:24 Mwandishi wa BBC Wanyama wa Chebusire anaripoti kuwa gari la mbunge mmoja wa zamani limeteketezwa moto katika kaunti ya Kakamega na watu wanaoaminika kuwa wafuasi wa mpinzani wake.
11:25 Mkuu wa Polisi David Kimaiyo asema kuwa takriban wanachama 200 wa kundi la MRC au Mombasa Republican Council walivamia kituo cha polisi wa doria wakiwa wanaelekea kusambaratisha shughuli za kupiga kura. Inaarifiwa polisi wanne
Tags
HABARI KIMATAIFA