Kikosi kazi cha zimamoto kutoka makampuni mbalimbali wakiwa kwenye sehemu ya juu ya ghorofa la PPF Tower lililopo Mtaa wa Ohayo (Ohio) eneo la Posta jijini Dar es Salaam baada ya kuwaka motoleo asubuhi, ambao chanzo chake bado hakijafahamika. Hata hivyo sehemu iliyowaka moto ni sehemu yenye mitambo mingi inayotumika kwa shughuli mbalimbali ndani ya jengo hilo.
Timu iliyodhibiti moto ikiendelea kuzima kabisa moto huo
Kama kawaida ya matukio mengi yanayotokea jijini Dar es Salaam mashuhuda hawakosi kama unavyoona pichani huku kila mmoja akitaka kushuhudia kinachoendelea.
Tags
HABARI ZA KITAIFA