WAJUMBE WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA KUAAPA KESHO

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898                            PRESIDENT’S OFFICE,

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com                  THE STATE HOUSE

press@ikulu.go.tz                                                                P.O. BOX 9120

Fax: 255-22-2113425                                                                 DAR ES SALAAM.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, atawaapisha Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Kesho tarehe 13 April, 2012, saa 3 asubuhi katika viwanja vya Ikulu.


Tume itaanza kazi zake rasmi tarehe 1, Mei, 2012 kama ilivyopangwa na kutangazwa awali.

Kwa kuzingatia umuhimu wa shughuli hii, Nawaomba wahariri mtutumie majina ya waandishi waandamizi ambao watafika ikulu mapema saa 2.00 asubuhi kwa ajili ya shughuli hii.

Tunaomba majina hayo ya wawakilishi wa vyombo vyenu yawasilishwe kwetu mara baada ya kupata taarifa hii na mwisho wakupokea majina itakuwa  saa 12.00 jioni ya leo .

Tunapenda kusisitiza kuwa waandishi watakaoruhusiwa kuhudhuria shughuli hii ni wale tu ambao tutapokea majina yao kutoka kwa wahariri wa vyombo husika.

Tunaomba ushirikiano wenu na karibuni.

Imetolewa na Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi.

Ikulu-Dar-Es-Salaam

12 April, 2012

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post