Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika ligi kuu ya England.
Yaya Toure alitoka mapema kutokana na kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na David Pizzaro huku Balotelli akitolewa kwa kadi nyekundu.
Mara mbili Robin Van Persie aligonga mwamba huku mkwaju mwingine aliopachika wavuni ukiwa wa kuotea.
Arteta alipata mwanya katika dakika ya 86 kwa kuachia mkwaju umbali wa yadi 25.
Arsenal sasa wamerejea katika nafasi ya tatu, pointi mbili juu ya Tottenham walio nafasi ya nne.
Awali manchester United iliichapa QPR kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Old Trafford.
Shuti kali la Scholes lilihakikisha ushindi wa United
Man United sasa imefikisha pointi 79, City ikifuatia na pointi 71 ikiwa imesalia michezo sita kumalizika kwa ligi.
MECHI ZA LEO JUMATATU
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.