NIJUZE NIJUZE Author
Title: Arsenal yaizabua City 1-0
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika...

Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika ligi kuu ya England. Arteta

Yaya Toure alitoka mapema kutokana na kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na David Pizzaro huku Balotelli akitolewa kwa kadi nyekundu.

Mara mbili Robin Van Persie aligonga mwamba huku mkwaju mwingine aliopachika wavuni ukiwa wa kuotea.

Arteta alipata mwanya katika dakika ya 86 kwa kuachia mkwaju umbali wa yadi 25.

Arsenal sasa wamerejea katika nafasi ya tatu, pointi mbili juu ya Tottenham walio nafasi ya nne.

Schioles

Awali manchester United iliichapa QPR kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Old Trafford.

Shuti kali la Scholes lilihakikisha ushindi wa United

Man United sasa imefikisha pointi 79, City ikifuatia na pointi 71 ikiwa imesalia michezo sita kumalizika kwa ligi.

MECHI ZA LEO JUMATATU

  • Everton v Sunderland
  • Newcastle United v Bolton Wanderers
  • Tottenham Hotspur v Norwich City
  • Aston Villa v Stoke City
  • Fulham v Chelsea
  • About Author

    Advertisement

    Post a Comment Blogger

    Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

    Note: Only a member of this blog may post a comment.

     
    Top