Bao la Kyle Walker kutoka yadi 25 liliiwezesha Tottenham kupata ushindi katika uwanja wa nyumbani White Hart Lane, dhidi ya wageni Arsenal, katika mechi ya kusisimua sana kaskazini mwa mji wa London.
Mlinzi Walker aliweza kufunga bao hilo katika dakika ya 73.
Bao la kwanza la mechi hiyo la Tottenham lilifungwa na Rafael van der Vaart katika kipindi cha kwanza, baada ya kuupokea mpira kutoka kwa Emmanuel Adebayor.
Aaron Ramsey aliweza kusawazisha katika kipindi cha pili, baada ya kupata mpira kutoka kwa Alex Song.
Ingawa Wojciech Szczesny angeliweza kuokoa mkwaju wa Walker, ni lazima ikumbukwe kwamba aliweza kuzima mikwaju ya Adebayor na Jermain Defoe.
Gareth Bale alikuwa pia na nafasi ya kuiwezesha Spurs kufunga mkwaju wa tatu, lakini juhudi zake ziliangukia patupu.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.