Unknown Unknown Author
Title: WAZIRI MKUU AONGOZA KUZINDUA DUKA LA BOHARI YA DAWA (MSD), MPANDA, MKOANI KATAVI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la Dawa la Bohari ya Dawa (MSD), Mpanda mkoani Katavi...
Duka la MSD Mpanda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la Dawa la Bohari ya Dawa (MSD), Mpanda mkoani Katavi. Kutoka shoto mwenye shati la kijani ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Katavi, Peter Mselemu, Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Kanali mstaafu Raphael Muhuga. Wa tatu kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Duka la MSD Mpanda
Jiwe la Msingi.
Duka la MSD Mpanda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu wakifurahi wakiwa ndani ya duka hilo.
Duka la MSD Mpanda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo wakiwa meza kuu wakati wa uzinduzi wa duka hilo.
Duka la MSD Mpanda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa MSD.
Duka la MSD Mpanda
Mwonekano wa duka hilo la MSD, mkoani Katavi.

Na Mwandishi Wetu, KATAVI
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema utaratibu wa MSD wa kununua dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji litaboresha upatikanaji wa dawa na kupunguza gharama za kununua dawa kutoka nje ya nchi.

Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa duka la dawa la MSD, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, mkoani Katavi, ambalo linaifanya MSD kuwa na jumla ya maduka 7 ya dawa nchini.

Waziri Mkuu pia amesema kwa mwaka huu wa fedha shilingi Bilioni 251 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba ili kupunguza changamoto za uhaba wa dawa na kueleza kuwa shabaha ya serikali ni kufikia asilimia 95-100 ya upatikanaji wa dawa hadi itakapofika mwezi Juni, 2017.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bwana Laurean Bwanakunu ameeleza kuwa duka hilo wataliendesha kwa mwaka mmoja tu, na kisha kulikabidhi kwa Halmashauri ili iliendeshe na kuongeza mapatao yao.

Kwa upande wa upatikanaji wa dawa, Bwanakunu amesema kuwa kwa sasa fedha sio tatizo, na dawa zinaendelea kuagizwa kulingana na mahitaji.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUWA KARIBU NASI LINDIYETU.COM
Usipitwe!! Ungana na Familia hii kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata Infortainment zote!! Usikose kujiunga na Youtube channel yetu ili kupata Exclusive mbalimbali kali kutoka LindiYetu TV

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top