Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika mwamvuli wa Ukawa kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila, akilakiwa kwa shangwe na wananchi wa mji wa Tabora, wakati akipita kuelekea jukwaa kuu, wakati wa Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Septemba 5, 2015.
Aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mngeja akiuhutubia Umati wa wakazi wa Mji wa Tabora, waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Town School, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Septemba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na Mwenyekiti wake, Mh. Freeman Mbowe, wakati wakitoka kwenye Mkutano wa hadhara wa Kampeni, Mjini Tabora Septemba 5, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Fredrick Sumaye akisalimiana na Mke wa Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Town School, kuhudhulia Mkutano wa Kampeni, Septemba 5, 2015.
Umati wa wananchi wa Mji wa Tabora ukiwa kwenye Mkutano huo.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwasalimia wananchi wa Mji wa Tabora, Septemba 5, 2015.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe akiwasalimia wananchi wa Tabora.
"Mabadilikooooooo......"
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia na kunadi sera zake kwa wananchi wa Mji wa Tabora, wakati wa Mkutano wake wa Kampeni uliofanyika Septemba 5, 2015.
CREDIT : OTHMAN MICHUZI