LIGI KUU VODACOM imeendelea Leo hii na Mechi pekee iliyotoa mshindi ni ile ya kule Mkwakwani Jijini Tanga Coastal Union ilipoifunga Ndanda FC Bao 2-1.
Jijini Dar es Salaam, Simba wameendelea kwa Sare katika Mechi zao zote 3 tangu Ligi ianze baada Leo kubanwa 1-1 na Timu mpya iliyopanda Daraja Msimu huu, Stand United ya Shinyanga.
Huko Uwanja wa Sokoine, Mbeya, Azam FC, Mabingwa Watetezi, walitoka Sare 0-0 na Prisons.
Mechi pekee iliyotoa mshindi hii Leo ni huko Mkwakwani Jijini Tanga wakat Coastal Union ilipoichapa Ndanda FC Bao 2-1.
Jumapili, Mtibwa Sugar iko kwao Manungu kucheza ma Mgambo JKT na wana nafasi ya kutwaa uongozi wa Ligi wakishinda.
Mechi ya Pili kesho Jumapili ni Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam wakati Yanga watacheza na JKT Ruvu.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.