Unknown Unknown Author
Title: MKUU WA WILAYA YA NACHINGWEA AITAKA HALMASHAURI KUREJESHA MAENEO YA WAZI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na. Ahmad Mmow, Nachingwea. Mkuu wa wilaya ya Nachingwea, Rukia Muwango ameitaka halmashauri ya wilaya hiyo irejeshe maeneo yote ya wazi ...
Na. Ahmad Mmow, Nachingwea.
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea, Rukia Muwango ameitaka halmashauri ya wilaya hiyo irejeshe maeneo yote ya wazi yaliyovamiwa na kutumika kinyume cha matumizi yaliyolengwa.
Mazoezi NachingweaMuwango ametoa agizo hilo leo mjini Nachingwea kwenye uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayoweza kuzuilika kupitia mazoezi na michezo, uliofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine.

Alisema yeye kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo anatambua na anazotaarifa za kutosha kuwa maeneo mengi ambayo yalitengwa kwa ajili michezo na shuguli nyingine za umma yamevamiwa na kubadilishwa matumizi.
Mazoezi NachingweaHivyo ameitaka halmashauri hiyo irejeshe haraka kutoka mikononi mwa wavamizi. Katika hali inayoonesha kuwa mkuu huyo wawilaya amelivalia njuga suala hilo, ameitaka halmashauri hiyo ipeleke na kumkabidhi mikakati na taarifa za utekelezaji wa agizo lake haraka.

Sambamba na agizo hilo Muwango ameitaka halmashauri hiyo kutenga maeneo kwa ajili ya michezo. Akibainisha kuwa bila kuwa na maeneo itakuwa vigumu kufanikiwa kukuza michezo na kuibua vipaji mbalimbali vya wanamichezo.
"Pia mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya nakuagiza uwandikie wakuu wa shule za sekondari na walimu wa kuu wa shule za msingi warejeshe mbio za mchakamchaka kwenye shule zao, shule nyingi wanafunzi hawakimbii mchakamchaka. Jambo ambalo ni muhimu kwa afya na akili za wanafunzi, ila walimu wawe na usimamizi mzuri ili wanafunzi wasiathiriwe katika masomo na usalama wao," alisema Mwango.
Mazoezi NachingweaAkizungumzia umuhimu wa michezo na mazoezi, Muwango alisema licha ya kuimarisha, umoja, udugu na mshikamano.
Lakini pia mazoezi na michezo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo, utulivu na amani katika jamii.

Alibainisha kuwa chanzo cha baadhi ya migogoro katika baadhi ya jamii ni magonjwa ambayo yanawewza kuepukwa kwa kufanya mazoezi. Hata hivyo jamii husika hazitambui hilo. Badala yake inayahusisha magonjwa hayo na sababu zisizo na msingi. Ikiwamo uchawi. Ndipo huanza kunyoosheana vidole na kusababisha migogoro.
"Lakini mtu akiwa mgonjwa hawezi kufanya shuguli za kiuchumi na maendeleo yake mwenyewe, taifa na hata wanaomuuguza hawawezi kufanya kazi ambazo zingewaletea maendeleo," aliongeza kusema Muwango.
Mazoezi NachingweaMkuu huyo wawilaya alitoa wito kwa wananchi wilayani humo kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi bila kujali rika. Huku akiwaasa kuunda vikundi vya michezo na mazoezi. Kwasababu madhara ya kutofanya ni mazoezi ni makubwa, bali ni vigumu kuyabaini haraka.

Uzinduzi huo ambao ni utekelezaji wa agizo la makamo wa Rais aliyetaka kuwe na kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayozuilika kupitia michezo, uliandaliwa na ofisi ya mkuu huyo wa wilaya ya Nachingwea. Ambapo michezo mbalimbali ilichezwa, upimaji wa magonjwa na uchangiaji damu kwa hiari ulifanyika.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUWA KARIBU NASI LINDIYETU.COM
Usipitwe!! Ungana na Familia hii kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata Infortainment zote!! Usikose kujiunga na Youtube channel yetu ili kupata Exclusive mbalimbali kali kutoka LindiYetu TV

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top