Unknown Unknown Author
Title: HATIMAE KAULI YA AFANDE SELE YA "WASAFI WATAONEKANA WACHAFU" IMETIMIA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Msanii wa muziki wa hip hop kutoka Morogoro Afande Sele amesema leo tafsiri ya msemo wake ‘wasafi wataonekana wachafu’ ambayo aliitoa ...
Msanii wa muziki wa hip hop kutoka Morogoro Afande Sele amesema leo tafsiri ya msemo wake ‘wasafi wataonekana wachafu’ ambayo aliitoa siku za karibuni baada ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutangaza awamu ya kwanza ya majina ya watu ambao wanatuhumiwa kujihusisha na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Kauli hiyo ilitafsiriwa vibaya na mashabiki wa Diamond wengi wakidhani mkongwe huyo naye naamini kwamba WCB wapo kwenye sakata hilo.

Kupitia list mpya ya RC Makonda ambayo ameitoa Jana na kutaja majina ya watu wakubwa, Afande Sele ameweka bayana nini alikuwa anakimaanisha kwenye kauli yake hiyo.

“Juzi kati niliposema kuwa kwenye hili sakata la MAPAPA na MAPUNDA wa"Unga"kama kweli braza Paul yupo"serious"….basi hata wale WASAFI wataonekana WACHAFU….wenye akili zao timamu walinielewa vyema….lkn vibichwa panzi walitafsiri kiudaku na kichonganishi tu wakimaanisha neno wasafi na wale wasafi wao wa mbagala…nadhani sasa tumeanza kuelewana…..NAONA MBALI KWA DARUBINI KALI…..wacha ‘parry’iendelee,” aliandika rapper huyo Instagram.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUWA KARIBU NASI LINDIYETU.COM
Usipitwe!! Ungana na Familia hii kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata Infortainment zote!! Usikose kujiunga na Youtube channel yetu ili kupata Exclusive mbalimbali kali kutoka LindiYetu TV

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top